HARAMBEE STARS WASHUKA KWA ORODHA YA FIFA
Timu ya taifa ya wanaume ya Kenya, Harambee Stars, imeporomoka nafasi moja katika viwango vya hivi karibuni vya FIFA vilivyotolewa hapo jana , kutoka nafasi ya 110 hadi ya 111 (pointi 1181.92) duniani.
Kutofuzu kwa Kenya katika Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka 2023 kunaweza kuchukuliwa kama sababu kuu ya kuporomoka huko, kwani harakati za timu, kulingana na FIFA, zimeathiriwa na mechi zilizochezwa katika mashindano hayo, pamoja na Kombe la Mataifa ya Asia lililofanyika Qatar mwezi huu.
Msumbiji ambao wamepanda hadi nafasi ya 110 kwa mafanikio yao katika AFCON, ambapo walipata sare dhidi ya timu kubwa za Afrika kama Misri na Ghana.
Mwingine aliyepanda kwa kasi katika eneo la CAF ni Nigeria – waliofikia fainali za AFCON – ambao wamepanda nafasi 14 hadi nafasi ya 28, huku washindi wa mwisho Ivory Coast wakivunja rekodi na kuingia kwenye 40 bora duniani: nafasi ya 39 wakipanda nafasi 10.
Moroko, licha ya kutolewa katika raundi ya 16 ya AFCON, wameendelea kuwa timu bora barani Afrika, wakipanda nafasi moja hadi ya 12, na Senegal wakishangaza kwa kupanda nafasi tatu hadi ya pili kwenye bara hilo katika nafasi ya 17.
Kwa upande mwingine, Uganda imeendelea kuwa timu iliyo juu zaidi katika uKanda wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA).
Cranes wamepanda hadi nafasi 92 na kuwa kileleni mwa eneo la CECAFA na pointi 1246.88.
Taifa Stars ya Tanzania, licha ya kutopata ushindi tena katika Kombe la Mataifa ya Afrika, wamepanda nafasi mbili hadi ya 119 na pointi 1160.98.
Imetayarishwa na Nelson Andati
English 

























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































