LISHE HATARI YAWAUA 4 KITUI

Polisi katika eneo la Kyuso kaunti ya Kitui wanachunguza kisa ambapo watu 4 kutoka Kijiji cha Nganda wamefariki baada ya kula chakula kinachoshukiwa kuwa kibovu.
Akithibitisha vifo hivyo, OCPD wa Kyuso Edwin Otieno, amesema waathiriwa walikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wamekutana nyumbani wka mkazi mmoja eneo hilo ambako walishiriki chakula cha Pamoja, na kisha wakaanza kulalamikia maumivu ya tumbo.
Kulingana na Otieno, watu watatu walifariki wakiwa njiani kuelekea katika hospitali Kyuso level 4, wa nne akafariki alipokuwa akipokea matibabu na wengine watatu wanaendelea kutibiwa.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa