NTSA YATANGAZA MSAKO BARABARANI
Wasafiri wamehakikishiwa usalama wao barabarani hasa msimu huu wa Krisimasi, mamlaka ya usalama barabarani NTSA ikitangaza msako mkali dhidi ya madereva wanaokiuka sheria za trafiki.
Kwenye msako huo, NTSA itategemea mahakama tamba zitakazohakikisha kuwa madereva wanaokamatwa wanashtakiwa na kuhukumiwa papo hapo, mbali na utekelezaji wa vifaa vya kudhibiti mwendo.
Aidha, wakenya wameruhusiwa kurekodi video za maafisa wa trafiki wanaochukua hongo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































