#Local News

KNEC YAONYA KUHUSU USAJILI WA KCSE 2026

Baraza la Kitaifa la Mitihani nchini, KNEC, limeonya kuwa hakutakuwa na usajili wa kuchelewa kwa watahiniwa wanaotarajia kufanya mtihani wa KCSE mwaka 2026.

Kupitia taarifa, KNEC imesema usajili wa mtihani huo ulianza Februari 16 na unatarajiwa kufungwa rasmi Machi 31 bila kuongezwa muda zaidi.

Baraza hilo pia limeeleza kuwa mtihani wa KCSE wa mwaka 2026 utakuwa wa pili kutoka mwisho kufanywa chini ya mfumo wa elimu wa 8-4-4 kabla ya nchi kuhamia kikamilifu katika mfumo wa mtaala wa umahiri, CBC

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *