UHURU KUONGOZA MKUTANO WA JUBILEE
Rais mstaafu Uhuru Kenyatta anatarajiwa kuongoza mkutano wa kitaifa wa wajumbe wa chama chake cha Jubilee, mkutano unaotazamiwa kutoa mwelekeo wa chama hicho kuhusu uchaguzi mkuu wa mwaka 2027.
Duru zimearifu kuwa Kenyatta ameitisha mkutano huo katika maandalizi ya uchaguzi huo, ikiwemo kumtangaza aliyekuwa Waziri wa usalama Fred Matiang’i kama mgombeaji wa urais kwa tiketi ya chama hicho kwenye uchaguzi mkuu ujao.
Jeremiah Kioni ni katibu mkuu wa Jubilee.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































