VIONGOZI, MATAIFA YAPONGEZA UCHAGUZI WA PROF. OKOWA
Uchaguzi wa Prof. Phoebe Okowa kuhudumu kama jaji wa mahakama ya kimataifa kuhusu haki ICJ umeendelea kupongezwa na viongozi na nchi mbali mbali, akiwa ni mwanamke wa kwanza kutoka Kenya kuchaguliwa kwenye wadhifa huo.
Wa hivi punde ni mkuu wa mawaziri Musalia Mudavadi, spika wa bunge la kitaifa Moses Wetang’ula, katibu katika wizara ya masuala ya kigeni Korir Sing’oei na mataifa yakiwemo Colombia.
Prof Okowa anachukua mahali pa hakimu Abdulqawi Yusuf wa Somalia.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































