WAWILI MAHAKAMANI KWA UFUJAJI WA FEDHA WEST POKOT
Maafisa wawili wa zamani katika serikali ya kaunti ya West Pokot wanatarajiwa kufikishwa katika mahakama jijini Eldoret kufunguliwa mashtaka ya ufujaji wa shilingi milioni 296 zilizokuwa zimetengewa hazina ya ufadhili wa masomo.
Wawili hao waliokamatwa na tume ya maadili na kupambana na ufisadi EACC, walihojiwa hapo jana na kuzuiliwa kwenye kituo kikuu cha polisi jijini humo.
Msemaji wa EACC Eric Ngumbi, tume hiyo inawasaka washukiwa wawili zaidi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































