#Local News

WATU WENYE SILAHA WAUA MTU, NA KUIBA NG’OMBE 100 HUKO ISIOLO

Polisi wanasaka Kundi la watu wenye silaha ambao wamevamia kijiji cha Isiolo na kumuua mchungaji mmoja kabla ya kutoroka na ng’ombe 100.

Kulingana na Polisi uvamizi huo umefanyika usiku wa kuamkia leo katika eneo la Kambi Garba.

Genge hilo limempiga risasi mchungaji mmoja kifuani walipovamia boma na kumuua papo hapo kabla ya kuondoka na ng’ombe waliokuwa kwenye boma.

Eneo hilo ni miongoni mwa maeneo ambayo bado yanakabiliwa na tishio la wizi wa mifugo.

Imetayarishwa na Janice Marete

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *