STARS WALENGA KUJINUSURU NA TANZANIA
Timu ya taifa kwa wachezaji wasiozidi umri wa miaka 17 Junior Stars watamenyana na Tanzania katika awamu ya semifainali ya mashindano ya kufuzu dimba la klabu bingwa barani Afrika AFCON kupitia ukanda wa CECAFA, licha ya kichapo cha bao 1-0 dhidi ya wenyeji Ethiopia.
Licha ya kichapo hicho, Stars walimaliza wa pili katika Group A, kutokanna sare ya bao 1 dhidi ya Somalia, na ushindi wa magoli 2-1 dhidi ya Rwanda, na watakabiliana na mshindi wa Group B ambaye ni jirani Tanzania.
Matineja hao wangali na nafasi ya kufuzu AFCON U17 mwaka ujao nchini Morocco, iwapo watailaza Tanzania.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































