#Local News

28 WAJERUHIWA KWENYE AJALI NAKURU

Watu 28 wanauguza majeraha, 12 kati yao wakiwa katika hali mahututi baada ya kuhusika kwenye ajali katika eneo la Salgaa kwenye barabara ya Nairobi- Nakuru mapema leo.

Kulingana na shirika la Red Cross, basi hilo linalomilikiwa na kampuni ya Easy Coach lilikuwa likitoka Nairobi kuelekea Kisumu lilipogonga lori la kusafirisha mizigo na kusababisha ajali hiyo.

Red Cross imesema 12 hao walipelekwa haraka hospitalini ila 16 wakahudumiwa katika eneo la mkasa.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *