ABIRIA WAKWAMA NDANI YA GARILA ABIRIA KWENYE AJALI JOGOO ROAD

Baadhi ya abiria wamekwama ndani ya basi lilioanguka katika eneo la makutano buruburu kwenye barabara ya Jogoo Rd.
Basi hilo la kampuni ya Forward lililokuwa linaelekea katikati ya jiji la Nairobi kutoka mtaa wa kayole wakati lilipoanguka na kusababisha msongomano wa magari.
Maafisa wa polisi wa trafiki Pamoja na maafisa wa huduma za dharura kwa sasa wako kwenye eneo la tukio kwendesha shughuli za uokoaji na kudhibiti msongomano wa magari.
Hata hivyo hakuna aliyeripotiwa kuaga dunia.
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































