POLISI WA KENYA KUTUMWA HAITI NDANI YA WIKI – ASEMA RUTO
Mpango wa kuwatuma maafisa wa polisi nchini Haiti ungalipo licha ya kupingwa vikali na baadhi ya viongozi na mashirika ya kutetea hali za kibinadamu.
Haya ni kwa mujibu wa rais William Ruto akiongeza kuwa kenya ina uwezo wa kurejesha amani katika taifa la Haiti na kwamba maafisa hao watatumwa Haiti kulingana na mkataba wa makubaliano na baraza la usalama la umoja wa mataifa.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































