SERIKALI YACHUNGUZA UDUKUZI DHIDI YAKE
Serikali inaendeleza uchunguzi katika tukio la udukuzi dhidi ya tovuti za wizara za maji, usalama, afya, leba na elimu na kuathiri kwa muda utoaji huduma kwa wananchi hapo jana.
Katibu mkuu katika wizara ya usalama Raymond Omollo, amehusisha udukuzi huo na kundi la PCP@Kenya, akiutaja udukuzi huo kuwa uvunjaji wa sheria.
Udukuzi wa hivi punde na mashambulizi mengine ya mtandaoni dhidi ya tovuti za serikali yanaathiri moja kwa moja uchumi wa kidijitali.
Imetayarishwa na Anytony Nyongesa
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































