NATEMBEYA; TUSIJIUE TUKIKUMBWA NA MFATHAIKO
Shughuli ya kutafuta mwili wa mwanafunzi wa kidato cha tatu aliyezama katika mto wa Koitobos ingali inaendelea.
Kwa mujibu wa barua aliyoandika Mwanafunzi huyo inadaiwa kuwa alijirusha katika mto huo kutokana ka msongo wa mawazo.
Gavana wa kaunti hiyo George Natembeya amefika eneo la Tukio ambapo ameahidi kuwatuma wapiga mbizi zaidi kusaidia katika shughuli hiyo.
Natembeya aidha amewarai wakaazi kutafuta ushauri nasaha wanapokumbwa na mfathaiko badala ya kujitoa uhai.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































