ALIYEKUWA MPENZI WA MWANARIADHA REBECCA CHEPTEGEI DICKSON NDIEMA AMEFARIKI

Aliyekuwa mpenzi wa mwanariadha Rebeca Cheptegei Dickson Ndiema ameaga dunia
Hospitali ilithibitisha kuwa Ndiema amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika chumba cha wagonjwa mahututi (ICU) alikokuwa amelazwa.
Ndiema amefariki siku chache baada ya Cheptegei kufariki katika hospitali hiyo hiyo.
Ndiema alimvamia Cheptegei nyumbani kwake ambapo alimmwagia petroli na kumchoma moto ambao pia ulimjeruhi.
Imetayarishwa na Janice Marete