HAJA YA MAFUNZO YA HUDUMA ZA KWANZA YAIBUKA
Wakenya wamehimizwa kupata mafunzo ya kutoa huduma za kwanza ili kupunguza maafa wakati wa mkasa au ajali katika maeneo ya mashinani kama ile ya ndege iliyotokea katika eneo la Mosop kaunti ya Nandi wikendi iliyopita.
Jacobeth Jeptoo, mwanafunzi wa uuguzi aliyejitolea kutoa huduma za kwanza kwa waathiriwa wa ajali hiyo iliyowaua watu 6, amesema mafunzo hayo yatasaidia kuokoa maisha.
Mwanafunzi huyo amegonga vichwa vya habari kutokana na juhudi zake kujaribu kuokoa maisha ya waathiriwa wa ajali hiyo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 


































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































