ABAUTANI YA WAFUGAJI KAJIADO KUHUSU CHANJO

Mpango wa serikali kuwapa chanjo mifugo humu nchini umepigwa jeki baada ya wafugaji katika kaunti ya Kajiado waliokuwa wamepinga mpango huo kubadili msimamo na kusema wataruhusu mifugo wao kuchanjwa.
Wakizungumza kwenye kikao cha kuwahamasisha wafugajki katika eneo la Kimana Kajiado Kusini, wafugaji hao wamechukua uamuzi huo baada ya kupata ufahamu wa kutosha kuhusu mpango huo.
Wakati uo huo, wameitaka serikali kuendeleza hamasisho ili kuwafahamisha wafugaji kuhusu umuhimu wa zoezi hilo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa