VIJANA 100 WA MAGENGE LIKONI WAJISALIMISHA
Vijana 100 waliokuwa wakijihusisha na uhalifu wamejisalimisha kwa polisi huko Likoni, kaunti ya Mombasa, wakiahidi kuachana na uhalifu.
Kamanda wa Polisi wa Pwani, Ali Nuno, ameahidi kuwasaidia kupata njia mbadala za kujikimu, huku mashirika ya kiraia yakiwasihi kujiunga na vyuo vya TVET vinavyogharamiwa na serikali ya kaunti.
Serikali ya kaunti imeahidi kuwapa ajira wale watakaohitimu.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































