WANAHARAKATI WAKEJELI ‘MAIGIZO’ TANZANIA
Watanzania wanaelekea kwenye uchaguzi wa urais hii leo, huku mashirika ya kutetea haki za kidemokrasia yakimkosoa rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa madai ya ukiukaji wa haki hizo kutokana na hatua yake ya kuwafungia nje wawaniaji wa upinzani.
Wakiongozwa na kiongozi wa chama cha PLP Martha Karua, wameutaja uchaguzi huo kuwa maigizo na wala si uchaguzi.
Hata hivyo, tume ya uchaguzi nchini humo imesema iko tayari kuendesha uchaguzi huo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































