WAKENYA MILIONI 2.2 KUTIBIWA BURE, RAIS
Wakenya milioni 2.2 walio na mapato ya chini wamepata afueni ya matibabu baada ya serikali kutangaza kuwa itakuwa ikiwalipia ada za SHA ili kugharamia matibabu yao.
Tangazo hilo limetolewa na Rais William Ruto katika Ikulu ya Nairobi, akisema mpango huo utawawezesha walengwa kupokea huduma za matibabu bila malipo katika hospitali za humu nchini.
Kulingana na rais, mpango huo ni sehemu ya serikali kuimarisha mpango wa huduma za afya kwa wote UHC.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































