CHANGAMOTO ZA KPSEA, KJSEA
Mitihani ya kitaifa ya gredi ya 6 KPSEA na gredi ya 9 KJSEA inaingia siku ya pili hii leo huku changamoto kadhaa zikiripotiwa katika siku ya kwanza ya mitihani hiyo hapo jana.
Miongoni mwa changamoto hizo ni baadhi ya shule kukosa kuwasajili watahiniwa, huku wanafunzi katika shule ya Endikir kaunti ya Kajiado wakianza mtihani wao alasiri baada ya karatasi za mtihani kukosekana kwenye kasha la kuhifadhi mitihani.
Jumla ya watahiniwa milioni 3.4 wanafanya mtihani huo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































