SENETI YAMHOJI WAZIRI MVURYA

Waziri wa madini na raslimali za majini Salim Mvurya amehojiwa na kamati ya seneti kuhusu raslimali za madini katika kaunti mbali mbali.
Waziri huyo ametakiwa kutoa maelezo kamili kuhusu jinsi wakazi watakavyonufaika na asilimia 10 ya mapato yanayotokana na madini
Kwa upande wake, kiranja wa wengi katika bunge hilo Boni Khalwale, amelalamika kuhusu mahangaiko ya wachimba migodi nchini licha ya idara hiyo kuchangia pakubwa katika pato la taifa.
Imetayarishwa na: Antony Nyongesa
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































