KARANI WA BUNGE LA HOMA BAY ASIMAMISHWA KAZI

Karani katika bunge la kaunti ya Homa Bay Faith Apuko amesimamishwa kazi.
Kwa mujibu wa barua iliyoandikwa na spika wa bunge hilo Julius Gaya Apuko amesimamishwa kazi kwa madai ya matumizi mabaya ya ofisi ,ufujaji wa fedha katika utoaji wa zabuni.
Apuko hata hivyo atapewa nafasi ya kujitetea baada ya siku kumi kukamilika.
Imetayarishwa na Janice Marete