KAWI GHALI YAATHIRI AFYA, KILIMO
Kongamano la mawaziri wa kawi kutoka kaunti zote 47 linaendelea kwa siku yake ya pili katika kaunti ya Makueni huku gavana wa kaunti hiyo Mutula Kilonzo Junior akisema kwamba gharama ya kawi ni ya juu, na kwamba imeathiri utendakazi wa serikali hizo.
Kongamano hilo linalenga kujadili mwafaka kuhusu kawi safi nay a bei nafuu ili kupunguza gharama ya utengenezaji wa bidhaa na uendeshaji wa shughuli za kaunti.
Kulingana na gavana huyo, gharama ya kawi imeathiri hasa sekta ya afya na ile ya kilimo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































