INGONGA AILAUMU DCI, IPOA KWA UCHUNGUZI
Huku waathiriwa wa ukatili wa polisi wakisubiri haki, imebainika kwamba idara ya upelelezi wa jinai, DCI, na mamlaka ya kutathmini utendakazi wa polisi, IPOA, zimekosa kuwasilisha faili za uchunguzi kwa afisi ya mkurugenzi wa mashtaka ya umma ili kuwafungulia mashtaka polisi wanaodaiwa kukiuka sheria.
Akizungumza jijini Nairobi alipokuwa akizindua mtaala kuhusu mashtaka ya ugaidi, mkurugenzi wa mashtaka ya umma Renson Ingonga, amesema nyingi ya kesi ambazo hazijawasilishwa kwake na taasisi hizo zinawahusu maafisa wa usalama.
Ameonya kuwa hatua hiyo itawaacha waathiriwa bila haki na washukiwa bila kesi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 




























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































