DAWA 77 ZA KUUA WADUDU ZAPIGWA MARUFUKU
Waziri wa kilimo Mutahi Kagwe ametangaza kupigwa marufuku kwa aina 77 ya dawa za kuua wadudu shambani kutokana na sababu za kiusalama.
Katika ujumbe Mutahi anasema wamechukua hatua hiyo ili kuhakikisha kuwa dawa zinazotumika nchini ni salama kwa binadamu na kwa mazingira.
Hii ni baada ya ukaguzi ulioendeshwa na bodi ya kudhibiti matumizi ya dawa hizo kwenye zaidi ya aina 430 ya dawa baadhi zikipatikana kutokuwa salama kwa matumizi.
Imetayrishwa na Maureen Mukhobe
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































