MASENGELI AADHIBIWE KWA KUKAIDI AMRI ZA MAHAKAMA – WAKILI KHAMINWA

Hakuna aliye juu ya sheria, haya ni kwa mujibu wa Wakili John Khaminwa akimtaka Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi Gilbert Masengeli aadhibiwe kwa kutotii maagizo ya mahakama.
Kulingana na Khaminwa hakuna aliye juu ya sheria kukataa kimakusudi kuheshimu amri za mahakama.
Wakili huyo Mwandamizi amesisitiza kuwa amri za mahakama lazima zizingatiwe na wote na kuongeza kuwa yeyote atakaekaidi lazima akabiliwe na hukumu na kuadhibiwa kwa mujibu wa sheria.
Imetayrishwa na Janice Marete