JIANDAENI KWA MEZA KAVU, WAKENYA WAONYWA
Wakenya sasa watalazimika kujizatiti kununua vyakula kwa bei ya juu
katika siku za hivi karibuni kutokana na mfumuko wa bei ya vyakula na mifumo mibaya ya hali ya hewa.
Katika ripoti yake ya hivi punde kwa kamati bajeti, afisi ya inayosimamia bajeti bungeni imebashiri kipindi cha mvua iliyo chini ya wastani
inayotarajiwa kuanzia mwezi wa Oktoba hadi Desemba mwaka wa 2025, hali inayotarajiwa kuathiri uzalishaji wa mboga na vyakula vinginevyo.
Kati ya mwezi wa Juni 2024 hadi Agosti 2025, bei ya vyakula muhimu ikiwemo mboga, mafuta ya kupikia na sukari ilirekodiwa kuongezeka.
Hata hivyo, ripoti hiyo imeangazia kushushwa kwa bei ya mafuta huku bei hiyo katika soko la kimataifa ikiratibiwa kupanda.
Katika kipindi cha mapito ,bei ya mafuta taa ilishuka kwa 9.7%, diseli
5.7% na petroli ikashuka kwa 6.4%.
Hata hivyo, ripoti hiyo imeoonya kwamba mvutano wa kijiografia na
kisiasa hasa katika maeneo ya Mashariki ya kati inaendelea
kuhatarisha soko la nishati.
Sekta kama vile nguo na viatu, afya , migahawa na malazi pia
ilishuhudia kuongezeka kwa bei.
Imetayarishwa na Maureen Amwayi
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































