PROF. OKOWA ACHAGULIWA JAJI ICJ
Kenya imepiga hatua kubwa kwenye ngazi ya haki ya kimataifa baada ya Profesa Phoebe Okowa kuibuka mshindi katika uchaguzi wa kuwa jaji katika mahakama ya kimataifa kuhusu haki ICJ.
Profesa Okowa ambaye tayari ni mwanachama wa tume ya sheria ya kimataifa, amechaguliwa katika kura za baraza kuu la umoja wa mataifa UN na baraza la usalama, na sasa atachukua wadhifa ulioachwa na hakimu Abdulqawi Yusuf wa Somalia.
Okowa atakuwa mwanamke wa kwanza mkenya kuhudumu kwenye mahakama hiyo ya ICJ.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































