#International

KENYA YATEULIWA RASMI NA MAREKANI KAMA MSHIRIKA MKUU ASIYE WA NATO

Rais wa Marekani Joe Biden ameteua rasmi Kenya kuwa mshirika mkuu asiye wa NATO.

Uteuzi huo unajiri wiki chache baada ya ziara ya kitaifa ya Rais William Ruto nchini Marekani.

Ni wakati wa ziara ya serikali ambapo Biden ametangaza nia yake ya kuwa na Kenya kama mshirika mkuu asiye wa NATO.

NATO ambayo inawakilisha Shirika la Mkataba wa Atlantiki ya Kaskazini kwa sasa ina nchi wanachama 32, zinazoitwa washirika wa NATO.

Hatua hii ya kihistoria ya Biden inaashiria hatua muhimu kwa Kenya kwani inakuwa taifa la kwanza la Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara kupokea hadhi hii na la nne barani Afrika.

Nyingine ni Misri iliyotunukiwa na Rais wa zamani Ronald Reagan (1987), Morocco na George W. Bush (2004), na Tunisia na Barack Obama mwaka 2015.

Ikulu ya White House imesema jina hili la kifahari limetolewa na Marekani kwa nchi ambazo inadumisha uhusiano wa karibu na wa kimkakati wa kijeshi na ulinzi.

Imetayarishwa na Janice Marete

KENYA YATEULIWA RASMI NA MAREKANI KAMA MSHIRIKA MKUU ASIYE WA NATO

KITAELEWEKA BUNGENI LEO

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *