KUCO YATISHIA MGOMO
Muungano wa maafisa wa kliniki umetoa notisi mpya ya mgomo katika kaunti ya Mombasa kwa malalamishi kwamba gavana wa kaunti hiyo Abdullswamad Nassir anawakandamiza wanachama wa muungano huo.
Mwenyetiki wa kitaifa wa muungano huo Peterson Wachira amelalamika kwamba serikali hiyo imekosa kutekeleza mkataba wa maewalano ya kurejea kazini yaliyowekwa na mahakama ya uajiri na leba tarehe 9 mwezi jana.
Miongoni mwa malalamishi waliyoaibua ni kuhusu serikali ya kaunti ya Mombasa kukosa kuwalipa maafisa hao malipo yote ya miezi 3, na kuapa kuishinikiza kupitia mgomo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































