#Local News

MAWAKILI WASHINIKIZA KURA YA MAONI KUHUSU NG-CDF, NGAAF

Mswada wa marekebisho ya katiba wa mwaka 2025 uliopitishwa na wabunge ili kuzijumuisha kisheria hazina za NG-CDF, ile ya uangalizi ya maseneta na NGAAF kwenye katiba umeibua ukosoaji nchini, kundi la mawakili likishinikiza marekebisho hayo kufanywa kupitia kura ya maoni.

Mawakili hao wameliandikia bunge la kitaifa na seneti kuhusu msimamo wao, wakishikilia kuwa kupitishwa kwa mswada huo ambao sasa unasubiri kuidhinishwa na maseneta, utabadili muundo wa serikali.

Wametishia kuelekea mahakamani kupinga mchakato huo.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

MAWAKILI WASHINIKIZA KURA YA MAONI KUHUSU NG-CDF, NGAAF

SI MIMI WALLAHI, ALAI

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *