WATAKAOCHOKOZA POLISI WAONYWA
Wakenya watakaojitokeza kushiriki maandamano ya hapo kesho wameonywa dhidi ya kuwadhalilisha ama kuwachokoza polisi.
Rais William Ruto anasema watakaofanya hivyo watakabiliwa na mkono wa sheria na kuwa jukumu la polisi ni kuimarisha doria na kuweka mazingira na ulinzi kwa waandamanaji.
Naye waziri wa usalama Kipchumba Murkomen ametaka kuchukuliwa hatua watakaotishia kuvamia idara na taasisi za serikali.
Imetayrishwa na Maureen Mukhobe
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































