WAGOMBEAJI WA KASIPUL WATOZWA ADA KWA KUSABABISHA MACHAFUKO
Tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC imewatoza faini ya shillingi million 1 wagombeaji wa eneo bunge la kasipul Body Were na Philip Aroko kufuatia makabiliano mabaya yalityosababisha vifo vya watu wawili .
Baraza la uchaguzi limesema kuwa adhabu hiyo inafaa kulipwa chini ya saa 48 huku wawili hao wakipewa onyo kali na kuhimizwa kuwa mstari wa mbele katika kudumisha amani eneo hilo.
aidha IEBC imesema kuwa uchaguzi wa eneo hilo utaendelea kama ilivyoratibiwa hapo awali kila mgombea akitakiwa kufuata sheria za uchaguzi .
Imetayarishwa na Jones Koikai
English 
























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































