#Sports

JOBE BELLINGHAM AJIUNGA NA DORTUMUND

Borussia Dortmund imemsajili kiungo wa kati wa Uingereza Jobe Bellingham kutoka Sunderland hadi 2030, miaka mitano baada ya kumleta kaka mkubwa Jude katika klabu hiyo.

Inasemekana kwamba Dortmund ililipa ada ya takriban euro milioni 33 (dola milioni 37), na bonasi milioni tano za ziada ili kupata huduma ya kiungo huyo, pesa nyingi zaidi klabu imelipa kwa mchezaji.

Baada ya kuondoka Birmingham City, Jude alikaa Dortmund kwa misimu mitatu na amekuwa mmoja wa wachezaji wanaotambulika zaidi katika soka la dunia tangu ajiunge na Real katika 2023.

Jobe alifunga mabao manne na kutoa pasi tatu za mabao katika mechi 40 alizoichezea Sunderland msimu huu na kuisaidia klabu hiyo kupanda Ligi Kuu.

Kusajiliwa kwa Jobe kunamaanisha kwamba huenda ndugu wawili jude na jobe wanaweza kumenyana katika michuano ya Kombe la Dunia ya Klabu iliyopanuliwa msimu huu nchini Marekani, ikiwa Dortmund watakutana na Real Madrid wakati wa miondoano ya kinyang’anyiro hicho.

Jude Bellingham alijiunga na Dortmund kutoka klabu ya utotoni ya Birmingham mwaka 2020 akiwa na umri wa miaka 17 kwa takriban euro milioni 23, ada ambayo ilipanda hadi euro milioni 30 wakati ada ya mauzo ilipoongezwa baada ya kuhamia Real Madrid kwa euro milioni 100.

Alicheza mechi 132 akiwa na rangi ya njano na nyeusi, akifunga mara 24 na kutoa pasi za mabao 25, na kuwasaidia kushinda Kombe la Ujerumani mwaka 2021 pamoja na Erling Haaland na Jadon Sancho.

Baada ya kuondoka Dortmund, Jude alikabiliana na timu yake ya zamani kwenye fainali ya Ligi ya Mabingwa ya 2023-24, na Real kushinda 2-0 Wembley.

Jobe alikua mchezaji wa pili mdogo wa Birmingham City nyuma ya kaka yake alipocheza mechi yake ya kwanza akiwa na umri wa miaka 16 na siku 107.

Imetayarishwa na Nelson Andati

JOBE BELLINGHAM AJIUNGA NA DORTUMUND

STARLETS WATUA VYEMA JIJINI DAR

JOBE BELLINGHAM AJIUNGA NA DORTUMUND

ROBO FAINALI YA WAVU YAHAIRISHWA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *