POLISI ‘WALIOMDHULUMU’ MWANGI KUZUILIWA ZAIDI
Maafisa wawili wa polisi ambao ni Klinzy Masinde na Duncan Kiprono wanaotuhumiwa kumpiga risasi mchuuzi Boniface Mwangi jijini Nairobi wataendelea kuzuiliwa kwa siku 15 zaidi ili kuruhusu uchunguzi dhidi yao kuendelea.
Mawakili wa maafisa hao hata hivyo umeiomba mahakama kuhakikisha kuwa simu za wateja wao zinalindwa wakati wa uchunguzi, upande wa mashtaka ukishikilia kuwa hakuna simu zilizonaswa.
Imetayrishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































