OGAMBA: SERIKALI INAJIKAZA KUMALIZA MGOMO WA WAHADHIRI

Serikali inajisatiti kuhakikisha wahadhiri wanaogoma wanarejea kazini, haya ni kwa mujibu wa waziri wa elimu Julius Ogamba akiongeza kuwa mazungungumzo yangali yanaendelea baina ya wahadhiri na serikali katika juhudi za kumaliza mgomo unaoendelea.
Kuhusu swala la matatizo yanayokikumba chuo kikuu cha moi mjini Eldoret Ogamba amesema kuwa ni jambo la kusikitisha kuona baathi ya wanafunzi wakikaa vyuoni hadi miaka 9 badala ya miaka minne kwa sababu za migomo ya mara kwa mara.
Ameahidi kuwa hilo litatatuliwa na hali ya kawaida kurejelewa.
Imetayarishwa na Janice Marete