ASANTE KWA KUNIAMINI! JUNET ANAMWAMBIA BABA BAADA YA KUCHAGULIWA KUWA KIONGOZI WA WACHACHE

Mbunge wa Suna Mashariki Junet Mohamed amemshukuru kiongozi wa Azimio Raila Odinga kwa kumteua kama kiongozi wa Wachache katika Bunge la Kitaifa.
Junet amethibitisha kuwa chini ya uongozi wake, vuguvugu lao litaibuka na ushindi
Matamshi yake yalijiri baada ya chama cha ODM kuafikiana na Mbunge wa Suna Mashariki kuwa kiongozi wa Wachache.
Junet, ambaye anahudumu kwa muhula wake wa tatu, atakuwa akichukua nafasi ya kiongozi wa Wachache anayeondoka Opiyo Wandayi ambaye ameteuliwa kuongoza hati ya Nishati na Petroli katika serikali pana ya Rais William Ruto.
Imetayarishwa na Janice Marete