WATU 7 WA FAMILIA WAFARIKI KWENYE AJALI HUKO NAIVASHA
Polisi huko Naivasha Kaunti ya Nakuru, wanachunguza ajali ya barabara ambapo watu saba wa familia moja wamefariki. Ajali hiyo imetokea katika barabara ya Naivasha-Longonot usiku wa kuamkia leo, ikisababisha vifo vya watoto wanne na watu wazima watatu. Miili ya marehemu imepelekwa katika hifadhi ya maiti ya Naivasha ikisubiri uchunguzi wa maiti. Imetayarishwa na Janice Marete
English 














































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































