#Local News

GACHAGUA ASEMA RUTO LAZIMA AONDOKE 2027

Aliyekuwa Naibu Rais, Rigathi Gachagua, amepuuzilia mbali mjadala unaoendelea kuhusu nani atakayekuwa mgombea mwenza wa Rais William Ruto katika uchaguzi wa 2027, akisema mjadala huo hauna maana.

Gachagua amesema mjadala huo unalenga kupotosha Wakenya, hasa kutoka eneo la Mlima Kenya, na kuondoa umakini wao katika masuala muhimu yanayowahusu.

Aidha, ameongeza kuwa iwapo Ruto atamchagua Gladys Wanga au Oburu Oginga kuwa mgombea mwenza wake, Wakenya hawana nia na hilo, akisisitiza kuwa lengo lao kuu ni kumng’oa madarakani mwaka 2027.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

GACHAGUA ASEMA RUTO LAZIMA AONDOKE 2027

MIKAKATI YA RBA YA KULINDA PENISHENI

GACHAGUA ASEMA RUTO LAZIMA AONDOKE 2027

WETANG’ULA ATETEA HAZINA YA NG-CDF

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *