KENYA KUNUFAIKA NA USHIRIKIANO MPYA NA MAREKANI
Kenya inatarajiwa kunufaika zaidi na ushirikiano wake na Marekani kufuatia mkutano wa ngazi ya juu kati ya Waziri Mkuu wa Kenya na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Seneta Marco Rubio, jijini Washington DC.
Mazungumzo yao yamelenga kuimarisha usalama wa kikanda, kuharakisha mkataba wa biashara huru kati ya Kenya na Marekani, na kuunga mkono juhudi za amani Afrika, hasa DRC na Haiti.
Rubio ameahidi kuitembelea Kenya hivi karibuni kuendeleza uhusiano huo wa kimkakati.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































