#Local News

KENYA YAAHIDI KUWATUMA POLISI ZAIDI HAITI

Kenya imeahidi kuwatuma maafisa wengine 600 wa polisi katika taifa la Haiti wiki zijazo ili kushirikiana na wenzao waliotangulia katika kupambana na magenge ambayo yanadhibiti maeneo muhimu ya taifa hilo, likiwemo jiji kuu la Port-au-Prince.

Idadi hiyo itafikisha jumla ya polisi 1,000 walioahidiwa kuwasilishwa nchini humo kusaidia kurejesha utulivu, kwa ushirikiano na vikosi kutoka mataifa mengine ambayo yameahidi kuwatuma maafisa 1,900 wa polisi kwa pamoja.

Akizungumza baada ya kuwatembelea polisi wa Kenya nchini Haiti, Rais William Ruto amepongeza juhudi za polisi hao hadi sasa.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

KENYA YAAHIDI KUWATUMA POLISI ZAIDI HAITI

IEBC MPYA KUNGOJA ZAIDI KUTOKANA NA KESI

KENYA YAAHIDI KUWATUMA POLISI ZAIDI HAITI

MASAIBU YA GACHAGUA SI YA LEO, WAMUCHOMBA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *