RUTO AKUTANA NA MAWAZIRI
Rais William Ruto anafanya kikao na baraza la mawaziri, wakati ambapo wengi wa mawaziri wake wanalaumiwa kwa kushindwa kutekeleza majukumu yao, mbali na kujihusisha na ufisadi na ubadhirifu wa fedha za umma.
Kikao cha rais kimethibitishwa na msemaji wa Ikulu Hussein Mohammed.
Katika kikao cha seneti hapo jana, maseneta walitumia fursa hiyo kuwakosoa baadhi ya mawaziri na maafisa wakuu serikalini.
Samson Cherargei ni seneta wa Nandi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































