SERIKALI: UPINZANI UNAJIRUSHIA VITOZA MACHOZI
Serikali imeibua madai kwamba viongozi wa upinzani wamekuwa wakipanga vurugu kwenye mikutano yao kwa lengo la kuvutia huruma kutoka kwa wananchi ili wapate uungwaji mkono, hatua ambayo serikali inasema itakabiliana nayo kisheria.
Akizungumza siku moja baada ya mkutano wa viongozi hao kaunti ya Kakamega kutatizwa kwa vitoza machozi, Waziri wa usalama wa kitaifa Kipchumba Murkomen, amesema serikali itafanya kila iwezalo kuwakabili viongozi wa kisiasa wanaoendeleza vurugu taifa linapoelekea kwenye uchaguzi mkuu ujao.
Amesema idara ya usalama iko macho kuzima tishio lolote la kiusalama.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 







































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































