#Local News

IEBC YAMTEUA SUNKULI KUWA KAIMU CEO

Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka, IEBC, imemteua Moses Ledama Sunkuli kuwa Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu na Katibu wa Tume.

IEBC imesema kuwa Sunkuli, ambaye kwa sasa ni Mkurugenzi wa Operesheni za Uchaguzi, atahudumu kwa nafasi ya kaimu kwa kipindi cha miezi sita au hadi mchakato wa kuajiri afisa mkuu mtendaji wa kudumu utakapokamilika.

Nafasi hiyo iliachwa wazi baada ya Marjan Hussein Marjan kujiuzulu kufuatia makubaliano ya pande zote ya kusitisha huduma zake katika tume hiyo.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

IEBC YAMTEUA SUNKULI KUWA KAIMU CEO

TIMBER: ARSENAL WANA ARI YA UBINGWA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *