MILIMU ASEMA LEOPARDS WANA UWEZO WA KUBEBA TAJI
Aliyekuwa Meneja wa AFC Leopards, Joseph Milimu, ameitaka klabu hiyo yenye mataji 12 ya ligi
kuanza kujiamini kuwa ina uwezo wa kutwaa ubingwa wa KPL msimu huu.
Milimu amesema ushindi wa 1-0 wa Ingwe dhidi ya Gor Mahia katika Mashemeji Derby ulikuwa
tamko la nia, akisisitiza kuwa kikosi cha kocha Fred Ambani kina msingi madhubuti wa kuanza kupata
matumaini ya ubingwa.
Aidha, Milimu ameongeza kuwa hakuna timu iliyoonyesha ubabe wa moja kwa moja msimu huu,
jambo ambalo linawapa mabingwa watetezi, Police FC, nafasi nzuri ya kutetea taji lao.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































