RUKU AMKOSOA OGINGA KWA KUDAI WADHIFA WA NAIBU RAIS
Baadhi ya viongozi kutoka eneo la Mlima Kenya wamekosoa hatua ya kinara wa ODM Oburu Oginga kubadili msimamo na kutangaza kwamba chama hicho kinalenga wadhifa wa naibu Rais kama sehemu ya ushirikiano na chama cha UDA kwenye uchaguzi mkuu ujao, wakisema wadhifa huo utaendelea kushikiliwa na naibu Rais Kithure Kindiki.
Waziri wa utumishi wa umma Geoffrey Ruku ambaye amezungumza mjini Embu, amekariri kuwa kamwe hawataruhusu wadhifa wa naibu rais kuponyoka eneo hilo mwaka ujao.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 







































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































