UASU, KUSU KIBABII WAGOMA
Mgomo wa wahadhiri wa vyuo vikuu vya umma umelemaza masomo katika vyuo hivyo kwa siku ya pili, wahadhiri wakishinikiza kutekelezwa kwa mkataba wao na serikali kabla ya kurejea kazini.
Katika kaunti ya Bungoma, wahadhiri wa chuo kikuu cha Kibabii wamejiunga na wenzao kote nchini, wakisema serikali imekuwa ikiwahadaa kurejea kazini ila inakosa kutekeleza makubaliano.
Wafanyakazi wa chuo hicho chini ya muungano wa KUSU pia wamegoma.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































