IDADI YA WAFANYAKAZI VYUONI KUPUNGUZWA
Mamia ya wafanyakazi katika vyuo vikuu vya umma nchini wanakabiliwa na hatari ya kuachwa bila ajira baada ya serikali kutangaza kwamba haina uwezo wa kufadhili elimu katika vyuo hivyo.
Waziri wa fedha John Mbadi ametangaza kwamba serikali imeweka mpango wa kuvinusuru vyuo hivyo, ikiwemo kufunga baadhi ya mabewa na kupunguza idadi ya wafanyakazi ili kudhibiti mzigo wa fedha.
Tangazo la serikali kwamba haina fedha linakuja wakati ambapo vingi vya vyuo vinakabiliwa na madeni na changamoto za kifedha.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































