#Local News

MAHAKAMA YASITISHA UCHAGUZI WA KJSA

Mahakama kuu imesitisha kwa muda uchaguzi wa wanachama wa baraza la kitaifa la muungano wa wafanyakazi wa idara ya mahakama KJSA uliopangiwa kufanyika jumamosi.

Uamuzi huo umetolewa baada ya wafanyakazi watatu wa idara ya mahakama kuelekea mahakamani kupinga uchaguzi huo.

Vincent Gikunda, Oscar Soi Anthony Oniala na Frank Megiri waliwasilisha maombi ya kuwania nyadhifa katika baraza hilo kabla ya kukosa kujumuishwa kuwa miongoni mwa wawaniaji.

Imetayarishwa na: Janice Marete

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *